Sunday, May 18, 2014

KONGAMANO LA KENYA - 2014

    TANGAZO!!!

CHAMA CHA WANAFUNZI WA KISWAHILI VYUO VIKUU AFRIKA MASHARIKI
                                        (CHAWAKAMA)

KINAPENDA KUWATANGAZIA WANACHAMA NA WADAU WOTE WA KISWAHILI KUWA:

KONGAMANO LA KUMI (10) LA KIMATAIFA LA KISWAHILI NA MKUTANO MKUU LINATARAJIWA KUFANYIKA NCHINI KENYA TAREHE 21/08/2014 – 24/08/2014.

KUHUSU NCHI - KENYA

KUHUSU CHUO - LAIPIKIA

KUHUSU TAREHE - 25/08/2014 HADI 27/08/2014

KUHUSU SIKU YA KUWASILI- 24/08/2014

KUHUSU GHARAMA ZA KONGAMANO

·         MALAZI KWA SIKU NNE - TSH 12,000
·         CHAKULA -TSH 24,000
·         FULANA -TSH 15,000
·         CHETI CHA USHIRIKI -TSH 4,000
JUMLA YA GHARAMA = TSH 55,000

GHARAMA ZOTE HAPO JUU ZIKABIDHIWE KWA KIONGOZI WA TAWI KABLA YA 20/07/2014.

KUHUSU NAULI: KILA MSHIRIKI ATAJITEGEMEA KWANI MAZINGIRA YA MWANZO WA SAFARI YATATEGEMEA NA MSHIRIKI ANAKOSOMA AMA ANAKOISHI. ILA MCHANGANUO WA NAULI NI KAMA IFUATAVYO:

WASHIRIKI WATAKAOANZIA SAFARI DAR ES SALAAM, MOROGORO WANATAKIWA KUANDA TSH 134,000 KWENDA NA KURUDI, AMBAPO WASHIRIKI TOKA MBEYA WATATAKIWA KUUNGANA NA WASHIRIKI TOKA DAR ES SALAAM, MOROGORO, IRINGA, DODOMA, NA MIKOA JIRANI. KWA WASHIRIKI WA MWANZA TSH.114000 WAO WATATAKIWA KUPITIA MPAKA WA UGANDA HIVYO SI MUHIMU KWAO KUPITIA DAR ES SALAAM. Arusha tsh.54000 kwenda na kurudi.

KUHUSU HATI YA KUSAFIRIA (PASIPOTI)

KILA MWANACHAMA ANATAKIWA KUWA NA HATI YA KUSAFIRIA KATI YA HIZI:
Ø  HATI NDOGO (PASIPOTI NDOGO) TSH. 10,000
Ø  HATI KUBWA YA KUSAFIRIA (PASIPOTI KUBWA) TSH.50,000
KILA MMOJA ATALAZIMIKA KUFIKA OFISI ZA UHAMIAJI ZILIZO KARIBU NA MAKAZI YAKE ILI KUKAMLISHA MCHAKATO WA HUO.



           KAULI MBIU YA KONGAMANO NI
“KISWAHILI MALIGHAFI YA UMOJA WA AFRIKA MASHARIKI”

Kauli mbiu hii inalenga kuhimiza umoja na utangamano wa nchi za Afrika Mashariki.Lugha ya Kiswahili ina mchango mkubwa sana katika kuleta utangamano,umoja na mshikamano mwema baina ya nchi za Afrika Mashariki.Kando na mchango wa  Biashara,Michezo na Elimu.Swali ni je,Lugha ya Kiswahili ina mchango wowote katika mchakato wa kuimarisha na kukuza vipengele hivi vitatu; umoja,utangamano na mshikamano.

MADA ZA KONGAMANO

1.   Kiswahili ni lugha mwafaka ya umoja wa Afrika mashariki.
2.   Nafasi ya lugha ya Kiswahili katika tamaduni za nchi za Afrika Mashariki.
3.   Kiingereza au Kiswahili? Katika mwamko mpya wa Afrika Mashariki huru.
4.   Kiswahili na michakato ya kisiasa katika nchi za Afrika mashariki.
5.   Nafasi ya Kiswahili katika sanaa ya kisasa (Karne ya ishirini na moja).
6.   Mchango wa lugha ya Kiswahili katika upanuaji na uendelezaji wa elimu
      ya juu Afrika Mashariki.
7.   Kiswahili na uimarishaji wa usalama katika ubia Afrika mashariki.
8.   Changamoto za kisiasa,kiuchumi na kiusalama katika lugha ya Kiswahili,
9.   Ubunifu na talanta katika uzalishaji wa kazi mufti ya fasihi ya Kiswahili
                        Lugha ya Kongamano:

Lugha rasmi ya Kongamano ni Kiswahili. Makala yaliyoandikwa kwa Kiingereza yatakubaliwa tu iwapo hapana budi.wajumbe wanashauriwa kuanda makala yao katika lugha ya kiswahili
Ikisiri: Ikisiri za kati ya maneno 200-300 zitumwe kabla ya tarehe 30 Mei 2014 kwa Mratibu wa Kamati ya Maandalizi kupitia barua meme kwenye anwani ifuatayo:Billysakwa@gmail.com,AU Mhariri
Mkuu godwinalex664@yahoo.com (+255718252853) au kwa katibu mkuu wa chawakama Afrika mashariki Ahamadi Jumbe. Chawakama.am@gmail.com.
Makala: Makala kamili ya ikisiri zitakazokubaliwa yatumwe kwa Mratibu kwa baruameme kufikia tarehe 30 Juni 2014 kupitia anwani ifuatayo: Billysakwa@gmail.com
Ili kupata nafasi ya kuwasilisha makala uliyoandaa ni lazima.mjumbe atume ikisiri na hatimaye makala kamili ya mada aliyoandaa.Makala haya yatachapishwa katika chapisho la makala la kongamano kabla ya tarehe 15 Julai 2014 .utaratibu na mpangilio wa uwasilishaji utatolewa tarehe 30 Julai 2014.



                         “KISWAHILI MALIGHAFI YA UMOJA WA AFRIKA MASHARIKI











1 comment:

. said...

Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com