Monday, March 31, 2014

TUNZO YA USHAIRI

Malengo ya shindano hili ni: kumkumbuka mwanzilishi wa Tunzo hii, Marehemu Gerard Belkin,
kuuenzi mchango wa mtunzi na mwalimu mashuhuri wa Tanzania, Professor Ebrahim Hussein, na
kukuza fasihi na lugha ya Kiswahili kwa kuibua na kuendeleza vipaji vya watunzi.
Shindano litafungwa 30 Mei 2014. Washindi watatangazwa mwezi wa Agosti. Mshindi wa
kwanza atapata zawadi ya 2,000,000 /=. Mshindi wa pili atapata 1,300,000 /= na mshindi wa
tatu atapata 700,000 /=.

MASHARTI
1. Hili ni shindano la utunzi wa ushairi katika lugha ya Kiswahilitu.
2. Kwa mwaka huu, tungo zitakazoshindanishwa ni za aina mbili tu:  mashairi na nyimbo.
   Tenzi/Tendi na kazi za kinathari, kama riwaya au tamthilia, hazitahusika.
3. Kila mshiriki awasilishe mswada MMOJA tu wenye tungo TATU tu.
4. Tungo ziwe ni za mtunzi mwenyewe.
5. Tungo ziwe  mpya kabisa. Yaani, zisiwe zimepata kuchapishwa au kutiwa katika CD au
    kanda; kuchezwa jukwaani, redioni au katika televisheni, au kusambazwa kupitia katika
    mitandao.
6. Bahari zitakazoshindanishwa ni: Kundi A: Mashairi(ya Kimapokeo au Huru-masivina); B.
    Nyimbo:Za kimapokeo, k.m. Taarabu, au za Bongo fleva.
7. Kila utungo wa kimapokeo uzingatie kanuni za kijadi za utunzi, na usipungue beti 10 au
    kuzidi beti 15. Utungo wa wimbo, pamoja na kuzingatia kanuni zinazohusika, usipungue
    beti 3 wala kuzidi beti 10.
8. Utungo huru usipungue mishororo (mistari) 3 wala kuzidi mishororo 50.
9. Kila mshiriki awasilishe tungo za bahari au aina moja tu katika makundi A na B.
10. Mtunzi atachagua mwenyewe mada na maudhui ya utungo wake.
11. Tungo ziheshimu miiko ya kijamii na kimaadili.

MAELEKEZO MENGINE
1. Kila mshiriki aambatanishe ukurasa wenye maelezo mafupi yenye kuzingatia yafuatayo:
• Jina lake kamili, wasifu na sifa zake kwa ufupi (umri, jinsi, kazi, utunzi wake)
• Anwani ya posta/makazi, anwani-pepe, na namba ya simu ya mkononi
• Maelezo kuwa mswada ni kwa ajili ya Shindano la Ushairi la Ebrahim Hussein
2. Tungo zichapwe kwa kompyuta, upande mmoja wa karatasi, kwa kutumia herufi za ukubwa
   wa pointi 12, na kuacha nafasi moja na nusu baina ya mistari.
3. Tarehe ya mwisho ya kupokea miswada ni: 30/5/2014, saa 10 alasiri.
4. Miswada inaweza kuwasilishwa kwa mkono, kwa njia ya posta au kwa barua-pepe.
• Miswada itakayoletwa kwa mkono iwasilishwe katika ofisi ya Tuzo iliyoko katika jengo la
   TPH Bookshop, Mtaa wa Samora Na. 24, Dar es Salaam.
• Miswada  itakayowasilishwa  kwa  njia  ya  barua-pepe  itumwe  kwenye  anwani-pepe
   ifuatayo: tunzoushairi@gmail.com
• Miswada itakayoletwa kwa njia ya posta itumwe kwenye anwani ya posta ifuatayo:
  Mratibu, Shindano la Ushairi la Ebrahim Hussein, Mkuki na Nyota Publishers Limited,
  S.L.P. 4246, Dar es Salaam
  Kwa maelezo zaidi tembelea Tovuti yetu: www.ushairi.com au piga simu: 0652 02 82 07

No comments: