Sunday, August 18, 2013

KHAMZIA


KHAMZIA

Kuna tanzu mbili za ushiri wa Kiswahili na ambazo zimetokana na asili ya kiarabu. Tanzu hizi ni “takhamisa”na “khamzia”. Utungo wa takhamisa una mistari mitano. Ilivyo ni kwamba utungo huu hutungwa na watu wawili. Mshairi wa kwanza hutunga mistari miwili ya mwisho na yule wa pili hutunga mistari mitatu ya kwanza lakini kwa kutumia kina cha mstari wa kwanza kati ya ile mistari miwili iliyotungwa na yule mtu wa kwanza.

Lakini katika utungaji yahitajia kwamba ile mistari ya mwanzo itakayongezwa isiharibu maana iliyoukiliwa na kwamba iwapo ile mistari mitatu itaondolewa ile miwili ibaki na maana yake ile ya mwanzo.

Utungo wa hamziya wahitaji mambo matatu muhimu, kwanza kabisa utungo huu unakuwa ni mistari miwili miwili, pili utungo jinsi ulivyo mistari yake haigawanyiki katika vipande viwili. Tatu ni kwamba silabi ya mwisho ya mstari wa kwanza si lazima iwe sawa na silabi ya mwisho ya mstari wa pili, lakini silabi zake za mwisho katika mistari yote ya mwisho shurti zilandane au ziwe na urari. (makala za semina ya kimataifa ya waandishi wa Kiswahili III, fasihi 2003:64-65)

Mashari aina ya takhimisa na hamziya yana asili ya kiarabu na tathlitha au utatu umetokana na nyimbo za Kiswahili. Hamziya ni fasihi andishi ya kwanza ambayo ilitafsiriwa kutoka kiarabu mnamo mwaka 1652, kuhusu maisha ya mtume Muhamadi. Hamziya ilivumbuliwa huko pate. Ingawa hamziya ilitafsiriwa kutoka kiarabu lakini ina muundo wa kibantu na lugha iliyotumiwa ina misingi mikubwa ya familia ya kibantu. Ni wimbo kwa ajili ya mtume wa kiislam na uliimbwa kwanza kabisa huko Egypt katika karne ya 13.

No comments: